RonaldoLionelMessi

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Sunday, 16 June 2013

Charles James Kahela, Aliyenusurika Kuuawa kwa Bomu Arusha Amefunguka!

Posted on 23:42 by Unknown
MLIPUKO WA BOMU ARUSHA

Charles James Kahela

Bwana Charles James Kahela, mkazi wa Arusha hadi sasa anaona kama ni muujiza kwake kubaki hai,  kwani haamini na wala haelewi kwa nini yeye apone wengine wafe.
Akitoa ushuhuda wake kanisani, Bwana Charles alisema,

"Baada ya kutoka kazini niliamua kupitia kwenye mkutano wa Chadema ambao ndio ulikuwa unafikia mwisho na kwa sababu mahali pale palikuwa karibu sana na kwa bosi wangu, nikaamua ngoja nami nisipitwe niende kusikiliza chochote kutoka kwa mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Bwana Freeman Mbowe." Alifuta machozi, kisha akaendelea. 

"Wakati mkutano umefika mwisho na watu wakiondoa baadhi ya vitu uwanjani huku viongozi nao wakiowa wametoka jukwaani, nilisikia kitu kimerushwa nyuma yangu karibu kabisa na kichwa changu na kwenda kutua mbela ambako kulikuwa bado na watu wengi tu na watoto kadhaa. Nikasikia mlipuko mkubwa sana, baada ya muda nikaona watu wamelala chini na damu nyingi sana zikimwagika. Kweli ilikuwa ni hatari sana, sijawahi kuona tukio baya kama hilo. Muda si muda polisi waliwazingira viongozi wa Chadema kwa ajili ya ulinzi huku wengine wakianza kurusha risasi kuelekea upande wa wananchi waliokuwa wakitoa kipigo kwa mtu mmoja aliyedhaniwa kuonekana akirusha bomu. Ilikuwa ni hatari tupu. Ilinibidi kuvunja mojawapo ya mageti ya mbao ya nyumba jirani na kulala chini ili kukwepa risasi ambazo zilikuwa zilirushwa chini chini sana. Mpaka sasa hivi ninavyoongea bado mwilini  mwangu nasikia joto sana na kutetemeka." Alimaliza Bwana Charles.

Kwa mujibu wa taarifa ya habari ya Redio One Stereo ya saa 2:00 usiku, serikali ilisema kwamba mlipuko uliotokea kwenye mkutano wa Chadema ilikuwa ni bomu la kutupwa kwa mkono. Waziri wa Mambo ya Ndani Dr Emmanuel Nchimbi aliyasema hayo wakati alipowatembelea waathirika wa bomu hilo katika hospitali za Mount Meru, St. Elizabeth na Serani zote za Jijini Arusha.

Nao uongozi wa mkoa wa Arusha umewaomba wananchi kuweka pembeni itikadi zao za kisiasa na kushirikiana kuwabaini watu waliohusika na milipuko wa bomu 
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in | No comments
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata na Wenzao Waliowasambaratisha Morocco
    Unaweza kuielezeaje mechi hii ya Stars v Morocco?
  • Liverpool Waliompa Kipigo Norwich Hawa Hapa
      Huku Suarez akipiga hat-trick
  • If You Missed Some Games of The AFCON From S.Africa. Here Are Actions in Pictures For You.
  • These are the 5 Problems That Manchester United Should Fix in Defence
    As Written by HITC SPORT   The System Ultimately the formation that Sir Alex Ferguson chose to play in the match against Cluj worked becaus...
  • Gossips About Usher Raymond, Tiffany Evans & Robbi Kristina
    Usher Raymond The drama continues to unfold between Usher and his ex-wife , Tameka. Following separate interviews on " Oprah's  Nex...
  • Is News About Wayne Rooney True?
    Although United are understood to be prepared to dispense with Rooney this summer should the club receive an offer in excess of £20m for the...
  • John Terry – Guilty and Not Guilty…What’s the difference?
    John Terry – Guilty and Not Guilty…What’s the difference?
  • 52 Ponda backers jailed. By The Citizen
    Story By Rosina John The Citizen Correspondent Fifty-two supporters of Muslim cleric Ponda Issa Ponda board a Prisons Department bus at Dar ...
  • Azam FC date Liberian team. Via IPPMEDIA
    Tanzania representatives in the CAF Confederation Cup, Azam FC have booked a last 16 game against Liberian club Barrack Y.C.II.   The first ...
  • MANDELA'S WIFE THANKS WORLD FOR 'LOVE, GENEROSITY'
    Via AP JOHANNESBURG  — The wife of former South African President Nelson Mandela says that love and generosity from across the world have br...

Blog Archive

  • ▼  2013 (172)
    • ►  August (33)
    • ►  July (29)
    • ▼  June (40)
      • PICHA HIZI ZINADHIHIRISHA KUWA WANA AFRIKA YA KUSI...
      • Hali Ya Nelson Mandela Yaleta Utata Mtupu
      • Haya Ndiyo Aliyoyasema Shinji Kagawa!
      • CHADEMA Wafunguka Tena. Safari hii ni Kuhusu Ugaid...
      • Nelson Mandela in Critical Condition. As Written b...
      • Yalojiri Kwenye Mechi Kali ya Japan Dhidi ya Italy
      • Freeman Mbowe na Mwenzake Godbless Lema bado Wanas...
      • CHADEMA Walonga na Kusema: "Tutawapa Polisi Mkanda...
      • East African Affairs ministers meet in Arusha
      • Via IPPMEDIA: Wassira challenges Mbowe to name Sat...
      • Kama Ulikosa Matukio ya Mabomu Arusha, Tazama Pich...
      • CHADEMA Wafunguka. Unajua Wanasemaje? Fungua Usome...
      • United's David Moyes handed £60m transfer kitty by...
      • MANDELA'S WIFE THANKS WORLD FOR 'LOVE, GENEROSITY'
      • JAY-Z ANNOUNCES NEW ALBUM WITH SAMSUNG DEAL
      • Alimanusura Stars Wamuue Tembo!!! Ivory Coast Wat...
      • Charles James Kahela, Aliyenusurika Kuuawa kwa Bom...
      • Huyu Hapa ni Wilfried Zaha wa MUFC
      • RVP KEPTENI WA UHOLANZI
      • Unamfahamu Manuel Pellegrini, Bosi Mpya wa MCFC? H...
      • Real Madrid's Offer to Ronaldo
      • Kama Unataka Kujua Alichosema Cristiano Ronaldo Ju...
      • Cesc Fabregas Kadai Maisha ya La Liga ni Matamu, H...
      • Najua Unamfahamu Busta Rhymes wa Mamtoni. Sasa Som...
      • Busta Rhymes - #Twerkit (Remix) Ft. Nicki Minaj | ...
      • Umeiona Kmart Clothing Collection Ya Nicki Minaj? ...
      • Mourinho Alipoulizwa Kama Anamuhitaji Wayne Rooney...
      • Ushahidi wa Lionel Messi Kukwepa Kulipa Kodi Huu H...
      • Huu Hapa ni Ushahidi Kwamba Lewandowski Katia Dole...
      • Manchester United Wammulika Thiago Alcantara
      • Videos | TJ Boyce - It's On | Nayo mpyaa!
      • Videos | RaVaughn - Best Friend | Mpyaaaa Kabisa!
      • Glenn Lewis - Can't Say Love. Ni Mpya Hii.
      • Jay-Z Ampa Skylar Diggins Benz Kama Zawadi ya Gra...
      • Is Tatyana Ali Dating Drake?
      • D'You Want to Know What Kelly Price Is About to Do?
      • Joe Thomas Akifunguka; Pia Kuhusu Album Yake Mpya.
      • Fabregas Kusaini Manchester United ama Arsenal?
      • Mourinho "the happy one" Unataka kujua kwa nini? f...
      • Robert Lewandowski Haendi Bayern Munich
    • ►  May (10)
    • ►  April (9)
    • ►  March (28)
    • ►  February (6)
    • ►  January (17)
  • ►  2012 (128)
    • ►  December (47)
    • ►  November (18)
    • ►  October (48)
    • ►  September (15)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile