RonaldoLionelMessi

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Saturday, 29 September 2012

Roberto Di Matteo na Mechi ya Leo Dhidi ya Arsenal

Posted on 00:48 by Unknown
Pamoja na kwamba mwisho wa wiki hii unaonekana ni mgumu sana kwa kocha wa Chelsea Roberto Di Matteo, lakini yeye mwenyewe anasisitiza kwamba hatishwi wala kuogopeshwa jinsi timu yake inavyoonekana kwa nje, yaani mitazamo ya watu. 

Roberto Di Matteo

Kepteni wa Chelsea John Terry amesimamishwa na chama cha soka huko Uingereza kutocheza michezo minne kutokana na katabia kake alikokaonesha ka ubaguzi wa rangi dhidi ya Anto Ferdinand msimu uliopita.  

 Anton Ferdinand na John Terry

Anton Ferdinand

Ingawaje Di Matteo, hataruhusu hukumu maneno yoyote toka nje ya kuhusu Chelsea ili isije wasumbua wachezaji wake na club kwa ujumla. 

"Tunajiamini ," alisema Di Matteo kuhusu mechi yao na Arsenal mchana wa leo. "hivyo hatujali sana kitu gani watu huko nje hunena juu yetu. Ni lazima tujiangalie nguvu yetu juu ya mchezo na huo ndiyo mwenendo wetu."  

"Hivyo ndivyo nionavyo na nihisivyo. Siwezi kuwaza eti watu wengine wana maoni gani. Tunachoweza kufanya ni kuwaza ni namna gani tunacheza na tunavyojiheshimu na kujitunza. Lazima tujiweke kwenye hali nzuri. Na hata mwisho wa siku tunajua kwa hakika wapenzi wa timu pinzani hawatatupenda."

"Hayo ndiyo maneno yangu kwa ujula. Hivyo hatutapoteza nguvu nyingi kuwa na wasi wasi juu  ya nini wanawaza. Ni lazima tujifikirie wenyewe, tujaribu na kushinda mechi kwa timu yetu."  


Terry atakuwepo kwenye mechi ya leo, pamoja na kukosa siku kadhaa za mazoezi ili ahudhurie kesi yake huko Wembley. 

Di Matteo alisema kwamba kila kitu kitaendelea kama kawaida na kwamba atachagua timu yake kwa mujibu wa Emirates pekee. 

"Uchgauzi wangu mimi ni wa kawaida tu." Alisema Di Matteo. "Ninavyoweza kuona Terry yupo fit. kutakuwa na taratibu za kawaida tu. Itakuwa ni kazi yangu kuchagua timu itakayoipiga Arsenal." 

Terry ana uwezo wa kucheza vizuri tu bila kujali mambo ambayo inaonekana yatawachanganya wengine, na Di Matteo anaona hakuna chochote cha kupoteza leo. 

Wakati bosi wa Chelsea alieleweka kuchukua tahadhari kuzungumzia ishu za hivi karibuni, alimsifu kwa hasaka Terry na tabia yake kwa upande wa kazi awapo uwanjani. "Niwezayo kusema ni kazi yake awapo kwenye timu." Alisema Di Matteo.

"Siku zote yeye ni wa kwamba kuwasili. Ana jitihada sana na amekuwa ni mtumishi mzuri sana wa timu yake. 

Chelsea walianza Premier League vizuri na wapo kileleni, lakini Arsenal watakuwa ni wapinzani wao hatari sana kwa msimu huu.  

"Utakuwa ni mtihani mgumu, alikubali Di Matteo. "Arsenal siku zote ni mtihani mgumu, ni changamoto kubwa kwetu. Lakini na kwao pia itakuwa ni changamoto kubwa, kwani sisi ni timu ngumu na nzuri pia.  

Ingawaje Arsenal walimuuza Robin van Persie na Alex Song, Di Matteo alisema alitabiri kwamba wangekuwa ni tishio kwao tangu mwanzo. 

"Nilisema mwanzoni mwa msimu kwamba Arsenal wataleta changamoto kwenye ligi," alisema meneja huyo. "Sina uhakika kama kuna aliyeniamini, lakini hivyo ndivyo nilivyooona mimi, na sijabadili mawazo yangu."  

"Sidhani kama wana namna nyingine tofauti ya kucheza. Wanacheza kwa kumiliki sana mpira na kuutafuta wanapoupoteza, lakini  Lukas Podolski na Gervinho wamekuwa wakifunga magoli, na Santi Cazorla. Wanao wachezaji ambao ni tishio na wenye uwezo wa kubadilisha nafasi." Alisema Di Matteo.

Kama wewe ni mshabiki wa Arsenal au Chelsea, unasemaje kuhusu mechi ya leo?
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in | No comments
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • If You Missed Some Games of The AFCON From S.Africa. Here Are Actions in Pictures For You.
  • Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata na Wenzao Waliowasambaratisha Morocco
    Unaweza kuielezeaje mechi hii ya Stars v Morocco?
  • Liverpool Waliompa Kipigo Norwich Hawa Hapa
      Huku Suarez akipiga hat-trick
  • Who has the best squad for title race - United, City, or Chelsea?
    Who has the best squad for title race - United, City, or Chelsea?
  • Ndugu, Soma Hiki Kioja cha Soka Huko Nigeria!
    T imu nne za mpira wa miguu zimesimamishwa kucheza soka nchini Nigeria baada ya mechi zao kuleta matokeo ya utatanishi kwa mechi hizo kumali...
  • Aston Villa vs Newcastle United: Same boat, different engine. Via HITC SPORT
    Alan Pardew's side head to Villa Park just one point ahead of the home team in the league, but differing transfer windows will likely ...
  • Manchester United Transfer Rumours: Cristiano Ronaldo Deal Reportedly Close | Bleacher Report
    Manchester United Transfer Rumours: Cristiano Ronaldo Deal Reportedly Close | Bleacher Report
  • Hatimaye Lulu Aliona Jua.
    Yule msanii maarufu sana hapa nchini kwenye tasnia ya filamu za bongo maarufu kama "Bongo Movie" Elizabeth maarufu kama "Lulu...
  • Pictures: Mario Balotelli's car gets pissed on and greased with bum sweat by Man United fans | 101GG Football news
    Pictures: Mario Balotelli's car gets pissed on and greased with bum sweat by Man United fans | 101GG Football news
  • Celtic Yawafanyia Kweli Barcelona
      Timu ya Celtic jana  usiku ilionesha kwamba Barcelona si chohcote kwao baada ya kuwatungua mara mbili kwa magoli yaliyowekwa kimiani na Wa...

Blog Archive

  • ►  2013 (172)
    • ►  August (33)
    • ►  July (29)
    • ►  June (40)
    • ►  May (10)
    • ►  April (9)
    • ►  March (28)
    • ►  February (6)
    • ►  January (17)
  • ▼  2012 (128)
    • ►  December (47)
    • ►  November (18)
    • ►  October (48)
    • ▼  September (15)
      • Liverpool Waliompa Kipigo Norwich Hawa Hapa
      • Picha 4 za Jinsi Man United Walivyokamatwa na Spur...
      • Spurs Yawachapa Kipigo Red Devils
      • Manchester United and Tottenham Hotspurs Clash His...
      • Eto'o Atangaza Kurudi Timu ya Taifa
      • Roberto Di Matteo na Mechi ya Leo Dhidi ya Arsenal
      • Arsenal Dhidi ya Chelsea Kesho
      • Why Cristiano Ronaldo Is the Tiger Woods of World ...
      • John Terry – Guilty and Not Guilty…What’s the diff...
      • Do You Know What Was Darren Fletcher's Dream?
      • John Terry is GUILTY in Racism Scandal
      • Wigan boss charged over post match comments agains...
      • Mourinho Could Manage Into His 70s: Originally Rep...
      • Rihanna with Her New Single "Diamonds"
      • 50 Cent Investigation
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile