RonaldoLionelMessi

  • Subscribe to our RSS feed.
  • Twitter
  • StumbleUpon
  • Reddit
  • Facebook
  • Digg

Wednesday, 20 March 2013

Lowassa afufua kashfa ya kigogo Ikulu. Kama Lilivyoandika Gazeeti la Mwananchi

Posted on 00:23 by Unknown


Dar es Salaam. Sakata la Mkuu wa Itifaki wa Ikulu, Anthony Itatiro, ambaye anahusishwa na njama za kutaka kuchota kiasi cha Sh3 bilioni kwa ajili ya safari hewa ya Rais, limechukua sura mpya baada ya Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje kutaka kujua hatima ya kigogo huyo jana.

Itatiro na maofisa wanne wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walituhumiwa mwaka jana kuidhinisha kuchota kiasi hicho cha fedha bila ya kuwapo kwa ziara ya Rais kwenda nchi yoyote ya kigeni.

Mpango huo unadaiwa kusukwa Juni mwaka jana kwa maofisa haokuitaka Wizara ya Fedha kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya safari hewa ya Rais.

Naibu Waziri wa wizara hiyo, Juma Mahadhi alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa swali na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge, Edward Lowassa.

Lowassa, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli aliuliza swali hilo ghafla kwa Mahadhi wakati akitoka nje, baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati yake kilichofanyika kwenye ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam.

Mahadhi, ambaye alilazimika kutoa ufafanuzi wa swali hilo baada ya kubanwa zaidi na waandishi wa habari, alisema Rais Kikwete ndiyo mwenye mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya Itatiro kutokana na ripoti ya uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mkaguzi wa Ndani wa Wizara hiyo.

Alisema pia kuwa walishauriwa kuwa maofisa walioshirikiana na Itatiro nao wachukuliwe hatua za kinidhamu kufuatia njama hizo.

Alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, Katibu Mkuu Ombeni Sefue hakupokea simu. Pia hakujibu pindi alipotumiwa ujumbe mfupi kwa njia ya simu. Naye Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais anayeshughulikia Utumishi, George Yambesi alisema hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwani alikuwa likizo.

Mahadhi alisema wakati tukio hilo linatokea viongozi wakuu wa wizara hiyo walikuwa kwenye majukumu mengine ya Serikali, jambo ambalo lilisababisha nafasi zao kukaimiwa na watendaji hao.

“Wale maofisa walitumia mwanya wao wa kukaimu nafasi ile ndiyo wakasuka mpango huo,” aliongeza Mahadhi.

Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya maofisa hao wamechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo ya kuwashusha vyeo na kuwabadilisha vitengo.

Mahadhi alisema kwamba huwa ni utaratibu wa kawaida kwa Rais anaposafiri maofisa wa Itifaki na wale wa Wizara ya Mambo ya Nje kupewa fedha na hazina kwa ajili ya kufanikisha ziara zake.
“Ila maofisa hawa walitumia mwanya huo kuihadaa Wizara ya Fedha kwa kuandaa hoja ya safari feki ili kupata fedha hizo,” aliongeza Mahadhi.

Maofisa wengine ni pamoja na ofisa katika Idara ya Itifaki, Shamim Khalfa, Kaimu Mhasibu Mkuu, Kasim Laizer, Mhasibu, Deltha Mafie na karani wa fedha) aitwaye, Shabani Kesi.
Source: Mwananchi
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest
Posted in | No comments
Newer Post Older Post Home

0 comments:

Post a Comment

Subscribe to: Post Comments (Atom)

Popular Posts

  • If You Missed Some Games of The AFCON From S.Africa. Here Are Actions in Pictures For You.
  • Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata na Wenzao Waliowasambaratisha Morocco
    Unaweza kuielezeaje mechi hii ya Stars v Morocco?
  • Liverpool Waliompa Kipigo Norwich Hawa Hapa
      Huku Suarez akipiga hat-trick
  • Who has the best squad for title race - United, City, or Chelsea?
    Who has the best squad for title race - United, City, or Chelsea?
  • Ndugu, Soma Hiki Kioja cha Soka Huko Nigeria!
    T imu nne za mpira wa miguu zimesimamishwa kucheza soka nchini Nigeria baada ya mechi zao kuleta matokeo ya utatanishi kwa mechi hizo kumali...
  • Aston Villa vs Newcastle United: Same boat, different engine. Via HITC SPORT
    Alan Pardew's side head to Villa Park just one point ahead of the home team in the league, but differing transfer windows will likely ...
  • Manchester United Transfer Rumours: Cristiano Ronaldo Deal Reportedly Close | Bleacher Report
    Manchester United Transfer Rumours: Cristiano Ronaldo Deal Reportedly Close | Bleacher Report
  • Hatimaye Lulu Aliona Jua.
    Yule msanii maarufu sana hapa nchini kwenye tasnia ya filamu za bongo maarufu kama "Bongo Movie" Elizabeth maarufu kama "Lulu...
  • Pictures: Mario Balotelli's car gets pissed on and greased with bum sweat by Man United fans | 101GG Football news
    Pictures: Mario Balotelli's car gets pissed on and greased with bum sweat by Man United fans | 101GG Football news
  • Celtic Yawafanyia Kweli Barcelona
      Timu ya Celtic jana  usiku ilionesha kwamba Barcelona si chohcote kwao baada ya kuwatungua mara mbili kwa magoli yaliyowekwa kimiani na Wa...

Blog Archive

  • ▼  2013 (172)
    • ►  August (33)
    • ►  July (29)
    • ►  June (40)
    • ►  May (10)
    • ►  April (9)
    • ▼  March (28)
      • Behind the charm, a political pope. Via Yahoo News
      • Britney Spears' Busy Vegas Weekend With New Beau. ...
      • Messi wastes late chance as Argentina held. Via Ya...
      • Justin Bieber Being Investigated for Battery. Via ...
      • Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata na Wenzao Waliowas...
      • Tanzania: All the Best to Taifa Stars. AllAfrica.c...
      • 52 Ponda backers jailed. By The Citizen
      • Luis Suarez to Quit Liverpool?
      • This is the Letter Written by Tomas Young, Iraq Wa...
      • Didier Drgba Nje ya Kikosi cha Ivory Coast
      • KAMA HUKUMFAHAMU 'Bosco Ntaganda' aka 'The Termina...
      • Bosco Ntaganda, ‘The Terminator,’ Surrenders to th...
      • IRENE MWAMFUPE JAMII: MNYIKA AITWA IKULU
      • IRENE MWAMFUPE JAMII: Polisi wazidi ‘kumchimba’ an...
      • IRENE MWAMFUPE JAMII: SHILOLE, BABY MADAHA WAFUATA...
      • Lowassa afufua kashfa ya kigogo Ikulu. Kama Lilivy...
      • Keyshia Cole Slams BeyoncĂ©, New Anthem on Twitter
      • Here is Justin Timberlake With His Long-awaited Th...
      • Here is Pope Francis the First
      • Justin Bieber's hamster has died. Via Mirror
      • This is What and How Barcelona Did to AC Milan
      • Is News About Wayne Rooney True?
      • Uhuru Kenyatta elected Kenya’s fourth president. V...
      • Hugo Chavez Died Hard
      • Azam FC date Liberian team. Via IPPMEDIA
      • ‘Form counts for nothing in Man U final’ - Soccer ...
      • Ryan Giggs – a global role model. Via The Telegraph
      • Vidic won't rule out Ronaldo return. Via Irish Exa...
    • ►  February (6)
    • ►  January (17)
  • ►  2012 (128)
    • ►  December (47)
    • ►  November (18)
    • ►  October (48)
    • ►  September (15)
Powered by Blogger.

About Me

Unknown
View my complete profile